N I wiki nyingine tunakutana tena kupitia ukurasa huu nikiamini kwamba umzima, bukheri wa afya na unaendelea nyema na maisha yako kama kawaida. Mimi niko poa kabisa tayari kukuletea mada nyingine ambayo naamini itakuwa ni yenye faida kubwa katika maisha yako ya kimapenzi. Mpenzi msomaji wangu, suala la kuoana si la kukurupuka, ni suala linalotakiwa kuchukua muda ambapo wawili waliotokea kupendana, hupata nafasi ya kuchunguzana katika mambo mbalimbali. Kabla ya kufikia hatua ya kuoana, ni lazima kwanza mtaanza kuwa marafiki wa kawaida. Kipindi hicho ndipo wewe utapata nafasi ya kubaini kama huyo uliye naye anastahili kuwa wako wa maisha. Mkishaona kwamba mmeridhiana kitabia, hapo mnaweza kuingia katika hatua ya uchumba na wakati huo penzi lenu halistahili kuwa la siri tena. Ndugu, jamaa na marafiki wanatakiwa kujua kwamba ninyi ni wanandoa watarajiwa! Elewa tu kwamba, kama utakutana na mtu kwa mara ya kwanza na akakueleza kwamba anataka kukuoa, atakuwa anakudanganya, na kama