KWENYE MAHUSIANO YAPO YA KUVUMILIANA LAKIN SIO HAYA
Neno uvumilivu lisitumike vibaya kiasi cha kuharibu mfumo wako wa maisha.. Kuna mengine hayavumiliki zaidi ya mara moja.. Kuna tabia zenye kuumiza na kukera unapo vumilia unafuga ubovu. Ukiona mtu mpenzi au rafiiki yako havumiliki kwa tabia zake usiogope kukaa nae mbali.. Huwezi vumillia kupigwa au kutukanwa hadharani. Huwezi vumilia mpenzi kukusaliti zaidi ya mara mbili zote anasema shetani alimpitia tu..alimpitia waende wapi? Huwezi endelea kuvumilia mtu asiye kuheshimu wala kukusikiliza hata mambo ya msingi. Kumbuka, Siku zote anaye penda na kujali sana katika mahusiano ndiye anayeishia kuumia. Wanasema mwenye upendo wa dhati hana bahati...unaweza mpenda sana mtu naye akajua ila yeye atapuuza hisia zako na kwenda kwa mwingine au kukusumbua makusudi akiamin kuwa huwezi muacha. Anapo taka kuachana nawe kamwe usimlazimishe kamwe abaki kwako. Kuna wakati bado una mhitaj ila yeye ameamua kuachana nawe huenda ameona amempata bora zaidi yako au amechoshwa na tabia zako. Nikwambie k