Posts

Showing posts from February, 2020

Muziki Ulimpenda BEN POL, Mapenzi ya MREMBO Kenya Yamempenda zaidi...

Image
BEN Pol bila muziki na kuwa staa, angeingiaje kwa mrembo wa kishua, Anerlisa Muigai? Mtoto ‘mkare' halafu ana kisu kikali, wazazi wake pia wana mawe ya kutosha. Ukiwa mwanamuziki mzuri huwezi kukosa wanawake wazuri wanaokuzunguka na kukutolea udenda. Ben ni mwanamuziki fundi. Ana uwezo mkubwa. Kama unabisha njoo tubishane. Ben ameshashinda sana kwenye muziki wake, ana bando lililosheheni ngoma kali. Ukinipa santuri yenye ‘misongi' yote ya Ben, nakuhakikishia sita'skip wala ku’forward. Zote ni tamu mwanangu! Unanipaje mtihani wa kusikiliza “Jikubali” halafu niache “Bado Kidogo”? Utanikuta nimeshasikiliza zote, halafu hutanifanya chochote. Masikio ni ya kwangu. Unakuja na mitego yako, eti unaniambia nichague kati ya “Pete” na “Maneno”, nakupa taarifa mapema kuwa nitatazama zote. Hulipii kodi macho yangu, ebo! Leta nyingine na nyingine kutoka kwa Ben, janki wa ugogoni hana kazi mbovu. Tangu Nikikupata, Samboira, Phone, Why, Wapo na nyingine zote unazozijua, mimi kaka yenu n

Ukitaka Usimegewe Hakikisha Unampa Mpenzi Wako Mahaba Niue Yenye Magawati za Kutosha

Image
Ukitaka Usimegewe hakikisha unampa Mpenzi wako Mahaba-Niue Niteketeze Kabisa yenye Megawati za kumtosha kuendesha Mitambo ya Furaha kwenye Moyo wake...Ukishindwa kumpatia lazima atakutafutia Jenereta la dharura au Solar Panel just incase Umeme-Penzi wako hautabiriki.Hakuna Mtu anayependa kukaa gizani kusubiria Umeme usiotabirika wa TANESCO wakati Majenereta yanauzwa. Ukitafutiwa Jenereta la Dharura kwenye Mapenzi usilalamike,Jilaumu mwenyewe kwa kutotabirika kwa Umeme-Penzi wako...Watu wanasikia Joto wameamua kujizatiti ili ukikatika tu kitu kinawaka AUTOMATIC. Shkamoo wote mliowekeza mitambo ya Symbion na Aggreko kwa sababu Wapenzi wenu wapo-wapo tu hawajitambui wanatumia Mita au Unit za LUKU WANAUME:Msipoangalia mtajikuta LUKU haina kazi mtu yuko under Generator masaa 24 kuepuka kadhia,Utajibebaje! By -Seth De Jesus

Nimekuta Chupi ya Kike Ndani ya Chumba cha Boyfriend Wangu, Yeye Asema Ajui ni ya Nani? Ushauri Tafadhali

Image
Wadau hapa nilipo nimechanganyikiwa na nisijue cha kufanya, naombeni ushauri wenu, nilikwenda field huko Tabora, nikamwacha mchumba wangu Tanga(ndiko kwetu) tulikuwa tukiwasiliana kama kawaida, na niliondoka nikiwa nimeshavishwa pete. Nilipigiwa simu baba yangu ni mgonjwa sana, watoto wake wote tulio mbali, tunatakiwa kurudi Tanga, basi nami nilirudi, na kukuta kweli hali ya baba si nzuri, nikampigia simu mchumba wangu kumuuliza yuko wapi, ili tukutane nae hospitali, akasema kwamba amesafiri kikazi gafla kwa siku moja tu then kesho yake angegeuza, nikamuuliza inakuwaje huniambii, akasema nimesafiri gafla, hata hivyo nilitaka nikujulishe maana nimeondoka leo. Niliumia sana kwa alichokifanya, sasa kuna rafiki yangu mmoja akaniambia, mbona mimi nimemuona jana super market? Akiwa na msichana? Nilijisikia huzuni sana ila nilijipa moyo nilikwenda moja kwa moja hadi kwake, nikamkuta mtoto wa mwenye nyumba, nikamuuliza kama kweli mchumba wangu amesafiri,(nikajua labda alikwenda supermarket

Silaha 5 za mwanamke kumteka mwanaume kimapenzi

Image
K ATIKA  maisha ya mapenzi watu wanapaswa kuelewana na kusikilizana mno. Hii ndiyo silaha kubwa zaidi kuliko zote na rahisi zaidi ya kukaa pamoja kwa muda mrefu. Pia mkisikilizana itasaidia wawili mnaopenda kudumu kwenye ndoa u uhusiano wenu hadi uzeeni. Ikitokea mwanamke akamsikiliza vizuri mwanaume wake na mwanaume naye akamsikiliza vizuri mwanamke wake, basi mapenzi ya watu hawa yanaweza kuwa mfano kwa watu wengine watakaotamani kuwa kama wao. Miongoni mwa vitu ambavyo watu wengi tunakosea kwenye mapenzi ni kujipa thamani na kujijali wenyewe zaidi kuliko wenzi wetu. Ni kosa kubwa! Jitahidi kumthamini mwenzio na huo ndiyo upendo wa dhati ambao hata Mwenyezi Mungu ametuagiza. Hata hivyo, wanawake wengi wamekuwa wakikosea baadhi ya vitu kwenye kumpata mwanaume na kudumu naye. Inawezekana imetokea hivyo kwa kujua au kutokuja kabisa, anajikuta tu uhusiano wake umekatika ghafla. Kwenye makala hii, leo nitawapa silaha tano ambazo mwanamke yeyote akiwa nazo atampata na kumteka mwa

Wanawake mnanisikia au niongeze sauti

Image
W ATAALAM  wa saikolojia na elimu ya uhusiano wa kimapenzi kati ya mwanamke na mwanaume, tunakubaliana kwa pamoja kwamba, wanaume ni viumbe rahisi mno kuridhishwa kwenye suala la unyumba au tendo la ndoa. Mwanzoni, kitu kinachomhamasisha mwanaume ni muonekano wako tu wa kimahaba (kwa mwanamke).   Lakini kadiri siku zinavyosonga mbele kwenye uhusiano, inakuwa ngumu kupandisha munkari wake, hata kama wewe ni mwanamke mrembo kiasi gani. Kumridhisha mwanaume wako inaweza ikawa rahisi kama tu utakumbuka kuweka mambo katika hali ya mvuto (remember to keep things interesting). Tafuta namna ya kuleta hamasa kama ile iliyokuwepo siku za mwanzomwanzo wa penzi lenu. Kwa uhakika utakamata usukani. Pamoja na kumheshimu, kama mtazingatia sheria zifuatazo kwa makini, basi mwanamke hatakuwa na shida ya kumridhisha mumeo. VAA VIZURI Utamu wa faragha unaweza ukawa kwenye tendo lenyewe, lakini matamanio ya kufanya tendo hilo, yanategemeana na mambo mengine mengi. Vaa vizuri wakati wa kulala, wa

Tabia za Msichana Anayekupenda Kimapenzi Lakini Anashindwa Kukuambia au Kukueleza!

Image
1. Atakutega kupata attention yako. Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda au lah! Mf wa mambo hayo ni kujifanya anaumwa na kuangalia respond yako kwake ni kiasi gani unamjali na kiasi gani utahangaika kwa ajili yake au 2. Haoni aibu kugusa sehemu yako ya mwili. Msichana anayependa haoni aibu kukushika mkono ama kukutomosa au hata kukumbatia. Kwa kufanya hivyo hujua kuwa kwa asilimia kubwa hisia za kushikana kwenu kutamrahisishia kazi ya kuwa na wewe 3. Kucheka kwa nguvu hata kwa kitu kisicho chekesha endapo wewe umezungumza. Mara nyingi ataonesha uso wa furaha hata kama si furaha ya kweli 4. Wivu. Hujisikia wivu anapokuona na wasichana wengine. Ukiwa unachart nao na ukiwaita majina ya kimahaba. Hapendi. 5 anakumbuka siku zako muhimu. Hukumbuka kama vile siku yako ya kuzaliwa hatowez kuisahau kufanya ipite bila kukutakia heri ya siku ya kuzaliwa kama sivyo ukifaulu mtihani au chochote katika maisha yako atakuwa mbele kukupongeza 6. Eye contact anapenda kukuangalia mach

Kila Msichana Ninae Mtongoza Ananiomba Hela...Whats This

Image
Mimi ni Kijana wa miaka 25 ninafanya kazi bank moja hapa Mjini ..nimefikia umri wa kutafuta mchumba wa kuoa ila hawa mabinti sijui wakoje kila ninaye mtongoza haipiti siku ananiomba hela kwa visingizio mbali mbali na mimi demu akishaniomba hela design hii hapo hapo naona sio namuona kimeo ndio wale wale .... Kwani Mapenzi siku hizi lazima usambaze Hela kwanza ndio upendwe ama? Naomba ushauri

Mke Wangu Akitoka....Mfanyakazi wa Ndani Ananikalia Mikao ya Kunitamanisha

Image
Wanaume kweli tunakazi aisee..yaani hivi karibuni mimi na mke wangu tumepata mfanyakazi wa ndani mpya kutoka Iringa lakini imekuwa ni majaribu kwangu mwanzo mwisho pale wife anapotoka nyumbani na mimi kubaki nyumbani, Kasichana haka kabichi kabisa kananitego kwa mikao mbali mbali ya ajabu ajabu, mara kajifanye kudeki huku kana khanga moko....sometimes napatwa na muhemko nafikiria kukatafuna ila naionea huruma ndoa yangu changa...Wife akirudi nyumbani kanakuwa kapole kanavaa vizuri kabisa utadhani kashamba...... Naombeni Ushauri Jamani Nifanyaje?

Nimemfumania Mke wa Rafiki Yangu Kipenzi Guest House Akiwaa na Njemba Jingine Waki

Image
Katika hali nisioitegemea tumegongana ana kwa ana Gest mi na shemeji yangu wa karibu ambae mme wake tunafanya kazi pamoja. Mimi nikiwa nampeleka mgeni wangu kwenye chumba alichofikia mara ghafla chumba chumba cha pili mlango ulifungulia na kikatokea kichwa tu kugeuka tukagongana ana kwa ana huyo shemeji yangu ilichukua takriban sekunde 30 kukodoleana macho na baada kutoa salam sauti ya chini mimi niliingia chumba cha mgeni wangu kumuaga na kumtakia safari njema wakati natoka huku mwili ukiwa umekufa ganzi kwa kutoamin nilichokiona kwa shemeji yangu na kutambua alienipokea zamu ya lindo saa 12 jion mke wake ana madudu niliishiwa nguvu kabisa, alikuja mhudumu wa ile Gest akaniitia chemba baadae akaja jamaa ambae sikuweza kumtambua kutokana na mazingira na kunieleza kilichotokea muda mfupi uliopita anaomba iwe niifanye kuwa siri kwanza ametokanae mbali isitoshe ni mzazi mwenzie na akanikabidhi elfu 70 ambayo mi nilikataa kuipokea huku nikimwambia kwasasa nahitaji kuwahi nyumbani mambo

Mpenzi Wangu Wakati wa Mechi Ananiulizaga ''Mpenzi Wangu Unataka nini Nikupatie'' Nimjibuje?

Image
Mpenzi wangu wakati wa mechi ; uwa mkimya lakini muda ukizidi kukolea akizdiwa wakati wa Uanza kuniuliza kwa kelele ''mpenzi wangu unataka nini nikupatie'' mimi uwa nashindwa jibu la kumpatia. Kwa vile ili swali amekuwa akiniuliza mara kwa mara , je nimpatie jibu gani?

Ukiyazingatia haya utaishi maisha bora ya kimafanikio

Image
Ni makosa kufikiri muda unaenda. Muda hauendi. Muda upo hapa mpaka mwisho wa dunia. Ni wewe ndo unaenda. Haupotezi muda, muda hauna mwisho. Unajipoteza mwenyewe, wewe una mwisho. Ni wewe unayezeeka, muda hauzeeki. hivyo tumia mda wako vizuri katika hii dunia. Namna mbaya sana ya kupoteza muda wako ni kujifananisha na wengine. Ng'ombe anakula majani na ananenepa, lakini Mbwa akila majani atakufa. Kamwe usijilinganishe na wengine. Kimbia mbio yako. Kinachomfaa mwingine kinaweza kisimfae mwingine. Tazama zaidi zawadi na kipawa alichokupa Mungu, na usiwe na wivu juu ya baraka walizopewa wengine. Kama ua rozi linanukia vizuri zaidi kuliko nyanya, haimaanishi kuwa rozi litatengeneza supu nzuri zaidi. Usijaribu kujilinganisha na wengine. Pia una uwezo wako, utafute na ujijengee uwezo zaidi. Wanyama wote duniani walikuwa kwenye safina ya Nuhu, na konokono ni mmoja wapo, Kama Mungu aliweza kumsubiri mpaka konokono aingie kwenye safina ndipo afunge mlango, mlango wako wa neema kamwe

Upendo unahitaji mambo haya

Image
Upendo unahitaji mambo yafuatayo ambayo ndio msingi wa upendo. Kuna vitu ambavyo upendo unahitaji; 1. Tumaini (Hope) Upendo unahitaji Tumaini, kwa lugha ya Kiyunani ‘elpis’ lenye maana ya (a) Favourable (b) Confident, expectation 2. Uvumilivu (patience) Upendo unahitaji uvumilivu kuvumiliana. Hakuna mwanadamu aliyekamilika katika mambo yote, unajua Waswahili wanasema “mvumilivu hula mbivu “ mvumilivu katika upendo maana yake hii ni shule ya kila siku, tunajifunza kutokana na makosa. Uvumilivu unatakiwa sana katika upendo - unajua kumfanya mwenzi wako kuwa kama wewe unavyotaka awe inahitaji uvumilivu. Hilo ni kweli, maana mmetoka mazingira tofauti na malezi tofauti; hivyo kumbadilisha inahitaji uvumilivu. 3. Kiasi Kiasi ni kitu muhimu. Chochote kinachofinywa zaidi ni hatari, unatakiwa uwe na kiasi katika mambo yako ili uweze kudumu katika upendo maana upendo unahitaji kiasi. Usijifanye uko (busy) sana unakosa hata nafasi/muda wa kukaa na mwenzi wako, lakini wewe unarudi usiku, h