Muziki Ulimpenda BEN POL, Mapenzi ya MREMBO Kenya Yamempenda zaidi...
BEN Pol bila muziki na kuwa staa, angeingiaje kwa mrembo wa kishua, Anerlisa Muigai? Mtoto ‘mkare' halafu ana kisu kikali, wazazi wake pia wana mawe ya kutosha. Ukiwa mwanamuziki mzuri huwezi kukosa wanawake wazuri wanaokuzunguka na kukutolea udenda. Ben ni mwanamuziki fundi. Ana uwezo mkubwa. Kama unabisha njoo tubishane. Ben ameshashinda sana kwenye muziki wake, ana bando lililosheheni ngoma kali. Ukinipa santuri yenye ‘misongi' yote ya Ben, nakuhakikishia sita'skip wala ku’forward. Zote ni tamu mwanangu! Unanipaje mtihani wa kusikiliza “Jikubali” halafu niache “Bado Kidogo”? Utanikuta nimeshasikiliza zote, halafu hutanifanya chochote. Masikio ni ya kwangu. Unakuja na mitego yako, eti unaniambia nichague kati ya “Pete” na “Maneno”, nakupa taarifa mapema kuwa nitatazama zote. Hulipii kodi macho yangu, ebo! Leta nyingine na nyingine kutoka kwa Ben, janki wa ugogoni hana kazi mbovu. Tangu Nikikupata, Samboira, Phone, Why, Wapo na nyingine zote unazozijua, mimi kaka yenu n