UNAPATA SHIDA KULALA? FANYA HAYA

Kubadili mwenendo wa kulala kunaweza kubadilisha mfumo wa mwili wa mwanadamu hali ambayo inasaidia kuimarisha afya, wanasema wanasayansi wa Uingerez na Australia.

Utafiti wao uliangazia zaidi ndege aina ya "bundi", ambao mfumo wa miili yao' huwezesha kuwa macho usiku kucha .

Mfumo huo unaweza kutumiwa kwa kuhakikisha mtu analala wakati mmoja kila siku, kuepukakunywa vinywaji vilivyo na caffeine kama vile chai na kupata mwanga wa jua hasa saa za asubuhi.

Watafiti wanasema mpangilio huo unaonekana kuwa wa kawaida lakini ni muhimu kwasababu unaweza kubadilisha maisha ya watu.

Kila mtu ana saa zake za kulala ambao unaambatana na kuchomoza na kuzama kwa jua. Ndio maana tunalala usiku.

Lakni mfumo wa miili ya watu wengine inatofautiana na watu wengine.

Kuna wale wanao amka mapema, lakini hawawezi kukaa macho kwa muda mrefu wakati wa usiku; na wengine wanaoweza kukaa macho kwa muda mrefu nyakati za usiku wakati kila mtu amelala.

Watu hao wanasemeka huenda wakapata matatizo ya kiafya

Post a Comment

0 Comments