MAHAKAMA YAAMURU WEMA SEPETU AKAMATWE

Na Karama Kenyunko, globu ya jamii.MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru msanii wa Filamu nchini, Wema Sepetu kumkamatwa  kwa kuruka dhamana.Wema anashtakiwa mahakamani hapo na kesi ya kusambaza  video ya ngono katika mitandao ya kijamii kupitia simu yake ya kiganjani. Mahakama imeto hati hiyo ya kumkamatwa Wema, leo Juni 11,2019  mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonda, baada ya upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Silvia Mitanto kudai kwamba mshtakiwa hayuko mahakamani na hakuwa na taarifa yoyote. Hata hivyo utetezi uliotokewa na wakili wa Wema, utetezi, Ruben Simwanza, ambae amedai mshtakiwa alifika Mahakamani lakini ameugua ghafla na hivyo ameshindwa kuingia katika chumba cha Mahakama, haukuweza kumsaidia Wema, na hivyo amri ya yeye kukamatwa ikatolewa.Akitoa uamuzi huo, jakimu Kasonde amesema Mahakama inatoa hati ya kumkamata mshtakiwa kwa sababu kama alifika alishindwa nini kuingia mahakamani. Katika kesi hiyo, Wema anakabiliwa na shtaka moja la kuchapisha video y... Continue reading ->

Post a Comment

0 Comments