QUEEN DARLING: 'KAMA KUDANGA NIMEDANGA SANA'

Dadake mfalme wa Bongo Flavour, Diamond Platinumz, Queen Darlene, amekiri kwa mara ya kwanza kuwa alikuwa akilala na wanaume wa umri mkubwa ili kupata pesa.

Mwanadada huyo ambaye pia ni mwanamuziki, amefichua kwamba alikuwa akiwategemea wanaume waliooa kujikimu kimaisha.

Akizungumza katika Wasafi FM inayomilikiwa na Diamond, Darlene alisema kuwa alikuwa akichumbiana na 'masponsa' kwa sababu alikuwa bado mchanga na kuhakuwa na ufahamu mwingi kuhusu maisha.

Kulingana na mwimbaji huyo, alijihusisha katika visa hivyo kwa sababu ilikuwa kawaida kwa wasichana waliokuwa katika umri wake.

"Wajua kuna wakati maishani ambapo wafanya kila utakacho kwa sababu ya kuwa bado mchanga. Ndio nilikuwa namchumbia mwanaume aliyekuwa ananizidi umri na alikuwa ananipa pesa lakini wakati huo ulipita. Na kwa sasa sitaki kulizungumzia suala hilo tena kwa sababu nina mpenzi ambaye ni wa umri wangu," Darlene alisema.

Ufichuzi wake unafuatia hali ambayo imekuwa ikimsumbua huku presha kutoka kwa mashabiki waliotaka kujua kama yey ni shoga ama ana matatizo katika kijinsia yake.

Mashabiki wake wengi wamekuwa na hisia mseto kuhusu uhusiano wake kwani hajawai kusema waziwazi ni nani mwanamume anayemchumbia.

Post a Comment

0 Comments