KILICHOMTOKEA HUYU BWANA NATANGAZA RASMI KUACHA “KUTONGOZA”


Kwanza nianze kwa kusema ' Shikamooni Wanawake wote Tanzania '.

Pili kama ningekuwa natakiwa Kugawa ' Tuzo ' ya Heshima leo hii ambayo ina hadhi ya Kimataifa basi ningempa huyu Mwanamke ambaye kwakweli kwa Kitendo chake cha ' Kimafia ' na ' Kishujaa ' alichokifanya leo mbele ya Baba mmoja mwenye tabia ya ' Kutongoza ' hovyo na ' Kumsaliti ' Mkewe basi haraka sana ningempa huyu Mama.

Tatu hivi ninavyotiririka na kuserereka kuwaandikieni hiki ' Kisa ' kilichotokea muda si mrefu maeneo ya Mbezi Beach ( ila kwa Maadili na Heshima ya Familia sitoweza Kutaja japo najua Wahusika wakiuona huu Uzi watajua ) ni kwamba huyo Baba yupo ' Mahututi ' na amelazwa mahala baada ya kupata ' Mshtuko ' mkubwa kwa kilichotokea na GENTAMYCINE kama mmoja wa ' Shuhuda ' wa ' Mtiti ' mzima nimejitahidi Kumuombea ili angalau Mwenyezi Mungu asiwahishe Kwanza Kufa au Kufariki Kwake ila naona maombi yangu kama vile ' Muumba ' bado hajayaafiki pengine nae ' amechungulia ' haraka katika Kitabu chake cha wenye ' Dhambi Tukuka ' na kakuta zangu ' hazivumiliki ' kabisa. Nimewaacha Watu wengine wakiendelea Kumuombea na Mimi nimejitoa kwa muda.

KISA KAMILI

Huyu Baba ( Mzee ) ana Heshima zake sana tu huko Mbezi Beach na tabia hii ya Kupenda Kutongoza tongoza hovyo Wake za Watu na Kutembea nao huku akijua wazi wazi kuwa ' anamsaliti ' Mkewe wa Ndoa leo amekutana na ' Picha la Kimafia ' ambalo hata Mimi GENTAMYCINE limenifanya niwe ' mpole ' kwa sasa.

Ni kwamba jana Usiku huyu Baba ( Mzee ) alienda Nyumba jirani kidogo na Kwake na Kumtongoza Mama mmoja hivi ambaye kwa bahati mbaya Kwake Mzee hakujua kuwa alikuwa na Uswahiba / Urafiki wa Kutukuka na Mkewe.

Mzee wa Watu baada ya kumwaga Voko / Sumu zake za ' Utongozaji ' yule Mama akamkubalia kuwa leo Saa 5 asubuhi wakutane ili wakachunjuane / wakatinduane / wakafanyane / wakangonoke / wakabanduane hivyo Mzee kama kawaida yake akaona amecheza kama Pele lakini hakujua kuwa kumbe yule Mama nae anacheza kama Zidane.

Huyu Mzee alipoondoka tu hiyo jana haraka sana huyu Mama aliyetongozwa akawahi kwa Mkewe na huyu Baba ' Tongoza Tongoza ' na kumwambia kuwa Mumewe amemtongoza hivyo sasa anataka amfanyie ' mchezo ' ili Mzee ' aumbuke ' ili ajifunze na aje kuacha rasmi hii tabia na atulie na Mkewe ( wenyewe mnasema abaki njia Kuu )

Yule Mama alipotoka tu kwa Mke wa huyu Mzee ( Baba ) akandaa sasa ' mazingira ' yote ile ' Tego ' litimie. Hivyo Mama akatafuta Chumba kimoja hivi pale Nyumbani Kwake Mbezi Beach ambacho kwa jinsi kilivyojengwa na kilivyo chenyewe hata mchana kama huu huwa ukiingia kinakuwa na Giza Kali na Kikifungwa Mapazia ndiyo kabisa kunakuwa sasa na Giza ' totoro '.

Mara baada ya kumaliza kuandaa hayo mazingira ' tengeneza fumanizi ' yule Mama akampigia yule Baba ( Mzee ) na kumpa maelekezo ya Kimasharti kwamba akienda leo pale aingie Mlango upi na aelekee moja kwa moja katika hicho Chumba cha mechi ya Kibaiolojia ya Simba na Yanga na akiingia humo ili kuwaficha Watu wengine wasijue kinachoendelea Yeye akiingia asiwashe taa bali atamwita kisha Yule Mama atakuwa tayari Kitandani ' ameshasalula ' na kubaki na Suti yake ya Asili ya Hawa ( namaanisha akiwa mtupu / uchi ) kisha Mzee Yeye avue zake na waanze ' Mziki '.

Baada ya ' Kusetiwa ' hivi huyu Mzee akajua kuwa kama kawaida yake Yeye ni Mshindi siku zote hivyo akajipanga kumbe wakati Yeye leo asubuhi amemuaga Mkewe anaenda Kazini muda ule ule Mkewe akakodi Bajaji na kwenda kwa Yule Dada ' Mafia ' kisha Yule Dada akampeleka huyu Mama katika Chumba kile kile ambacho alimuelekezea huyu Baba akifika tu aende kule moja kwa moja kisha huyu Dada Yeye akawa ' amejificha ' mahala kuona ' Picha ' kamali likiendelea.

Kweli muda ule ulipofika wa leo Saa 5 kama walivyoahidiana Yule Mzee ( Baba ) akaenda na akafuata yale maelekezo yote aliyokuwa amepewa awali ambapo alipofika tu ndani ya kile Chumba ambacho kina asili ya Giza aliingia na haraka akafunga mlango kisha Yule Mama ambaye ni Mkewe halali ' akaiigiza ' sauti ya Yule Dada ' Mafia ' ambapo Mzee kwakuwa alikuwa na ' minyegenyege ' yake ya Kipopoma / Kipumbavu wala hakujua kuwa aroboaini yake leo imefika.

Haraka haraka Mzee ' akasalula ' na Kupanda Kitandani huku ' Mkuyenge ' wake tayari ukiwa umeshasimama utafikiri Kifaru cha Idi Amini kinataka kurusha Kombora Kyaka Mkoani Kagera na akaanza sasa ' Shoo yake ya Kibabe '.

Kama kawaida yetu Sisi Wanaume huwa tukiwa tunajua kuwa leo tumepata Zigo Jipya / Demu Mpya huwa tunapenda kuonyesha ' mautundu ' yetu ya ' Kubandua ' kuliko hata vile ambavyo huwa tunafanya kwa Wapenzi wetu wa Kawaida ili mradi tuache tu ' Legacy ' ya ' Kubandua ' kwa Kutukuka.

Unaambiwa Mzee ( Baba ) aliisugua vilivyo ' Mbunye ' ya Mkewe halali huku Yeye akidhania anambandua Yule Dada ' Mafia ' hadi akawa anaisimamia kwa Kucha, anafanya ' manjonjo ' yake yote ambapo kwa mujibu wa Shuhuda kuna muda huyu Mzee kutaka tu kuonyesha kwamba Yeye ni ' Mtundu ' akiwa katika Mapenzi alipiga ' Sarakasi ' moja Kabambe hivi ambapo alipotua Kitandani Uume wake nao ' ukazama ' moja kwa moja Ukeni Kitendo ambacho tokea amuoe huyu Mama sasa mwaka wa 35 hakuwahi kumfanyia.

Alipomaliza sasa kufanya haya ' manjonjo ' yake yote huku ' Pumzi ' yake nayo kwa mbaali ikianza ' Kukata ' Mzee wa Watu akafanya ' Njonjo ' lingine ambalo lilizidi ' Kumkosha ' yule Mama na hatimaye akafika na Kujitupa Kitandani kama Mbuzi aliyeshiba Nyasi za Bonde la Mto Rufiji.

Ile alipomaliza tu lile ' Tendo ' na kujitupa Kitandani kwa ' Utamu ' aliompa Yule Mama ambaye ndiyo Mkewe halali ( japo Yeye alidhani ile shughuli yote alikuwa anamfanyia yule Dada Mafia ) ndipo Mama nae akamuambia haya maneno ambayo nayanukuu hapa na ambayo ndiyo yamemfanya Baba wa Watu hadi hivi sasa yupo ' Mahututi '.

" Mume wangu Baba nanihii....kumbe unajua Kufanya Mapenzi hivi sasa kwanini siku zote ulikuwa hunifanyi hivi? Asante kwa Penzi lako tamu na naomba uvae basi turudi Nyumbani ili tukafurahie zaidi Penzi letu kule "

Mara baada ya huyu Mzee ( Baba ) kusikia Sauti ambayo anajua ni ya Mkewe alishtuka na Yule Mama ( ambaye ndiyo Mkewe halali ) katika kutaka kumuonyesha kuwa ni Yeye haraka sana akaamka pale Kitandani na kwenda moja kwa moja ambapo alishaelekezwa na Yule Dada ' Mafia ' kuwa ' Kitufe ' cha Kuwasha Taa mule ndani kipo hivyo akaenda na akawasha ambapo Yule Baba akaona ni Mkewe kweli na hapo hapo ' akazimia ' kwa ' mshtuko ' mkubwa na wamemtoa pale walipokuwa wameenda kumpatia ' Tiba ' Kwanza.

Huu ndiyo ' Mtiti ' uliotokea leo maeneo ya Mbezi Beach ambao umefanya pia huyu Dada ' Mafia ' apongezwe na Wanawake wengi pale hadi na Wanaume baadhi japo Mimi GENTAMYCINE nilishindwa Kumpongeza / Kumkongole kwakuwa hata na Mimi leo hii Saa 10 nilikuwa na zoezi kama la Mzee na hata Mimi pia huyo ' Mlengwa ' nae ana Urafiki si tu wa karibu bali wa ' Kutukuka ' kabisa na Mke wangu Mama Junior hivyo na Mimi baada ya ' Kushuhudia ' hiki ' Kisanga / Kisa ' nimesitisha rasmi dhambi ambayo nilikuwa natarajia kwenda kuitekeleza, nimestaafu rasmi leo ' ukiwembe ' na sasa nitabaki tu na Mpenzi wangu Mama Junior hadi hapo labda Kifo kitakapotutenganisha.

Hili tukio liwe Funzo kwa Wanaume wenzangu wote!

Nawasilisha

BY GENTAMYCINE

Post a Comment

0 Comments