DAVINA ATOA NENO KWA WANAUME AMBAO HAWANA MSIMAMO

Muigizaji mkongwe Bongo Muvi, Halima Yahaya ‘Davina’ amefunguka kuwa hapendi tena kutumika kwa wanaume ambao hawana msimamo katika maisha yake dhidi ya kujizeesha.  

Davina amesema huko nyuma mtu unakuwa na akili ya kitoto hata unapokutana na mtu anakuambia anakupenda na kuamua kufunga ndoa nawe baada ya miezi kadhaa mnatengana.

“Sasa hivi jamani nimekuwa najitambua vilivyo na uzuri najua yupi anakudanganya au anakupendea umaarufu tu hivyo mambo ya kutumika bila mpango siku hizi hakuna tena kabisa,” alisema Davina.

(Visited 1 times, 1 visits today)

Post a Comment

0 Comments