FAHAMU ZAIDI KUHUSU UKOMO HEDHI

-Ukomohedhi ( Menopause) ni wakati mwanamke anapokosa kupata hedhi kawaida kwa muda wa miezi 12 mtawalia au mwaka mmoja

-Hali hii huwathiri wanawake wa umri wa miaka 40 ama wakati mwingine wa chini ya miaka hiyo

Dalili za Ukomohedhi

Dalili hizi hotofautiana kutoka mwanamke hadi mwingine na pia huchukua muda tofauti kukamilika.

Hii ni kwa sababu dalili hizi huchangiwa na kubadilika kwa mzunguko wa homoni kwa kila mwanamke.

7. Kupotea kwa Vifuko vya uzazi

Vifuko vya uzazi husaidia kuzalisha mayai ya mwanamke, na kusaidia katika mzunguko wa damu au kutungika kwa mimba baada ya mayai ya mwanamke kukutana na ya mwanamume.

Vinyweleo vya kifuko cha uzazi vikipotea hedhi nayo hukoma na pia kuwa vigumu kwa mwanamke kupata mimba.

6. Joto la ghafla mwilini

Mwili hupata joto kwa sekunde 30 mpaka dakika 10 hali ambayo huendelea kwa muda wa mwaka moja au miwili. Mwili hutokwa na jasho jingi usiku.

Ukomohedhi huleta mchanganyiko wa hisia. Picha:Facebook Health fitness and beuty

5. Kukosa Usingizi

Wanawake wengi wakikaribia umri wa kukosa hedhi, hukosa usingizi au kuamka mapema ama kushindwa kurejea usingizini baada ya kuamka.

4. Kuwa mkavu ukeni

Tatizo hili humfanya mwanamke kuhisi uchungu wakati wa kufanya mapenzi, kuhisi mkojo kila wakati ama kutoka kwa urahisi anapocheka, kufanya mazoezi ama kupiga chafya.

Hii ni kwa sababu mishipa ya uke hulegea na mwanamke huwa kwenye athari ya kupata magonjwa ya zinaa kama vile kisonono.

3. Kubadilika kwa hamu ya kufanya mapenzi

Muathiriwa anaweza kosa hisia za kufanya mapenzi, ama hisia hizo kuongezeka maradhufu kwa kuwa na hamu ya juu kutaka kujamiana.

2. Kubadilika kwa mudi

Anayekumbwa na hali hii anaweza kukosa kuwa na mudi wakati huu na dalili zake ni kukasirika haraka.

Hata hivyo bado wanasayansi hawajaweza kung'amua chanzo cha kubadilika kwa mudi namna hiyo.

1. Mwili kubadilika

Mwili huongezeka uzito. Kiuno kunenepa, kupungua kwa misuli, ngozi kukondeana, mifupa kukosa nguvu na pia kusababisha mwasho na kuwa mlegevu.

Bado watafiti hawajatambua kama dalili hizi ni za uzee.

Dalili hizi hutofautiana katika kila mwanamke na pia huchukua muda tofauti kukamilika.

Hii ni kwa sababu dalili hizi huchangiwa na kubadilika kwa mzunguko wa homoni za kila mwanamke.

Kulingana na wataalam, bado hakuna matibabu kamili kwa tatizo hili.

Hata hivyo kuna baadhi ya dawa zinazotumika kupunguza baadhi ya dalili kama vile maumivu ya mgongo na kichwa na dawa hizo hupatikana kwenye maduka ya dawa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke; obed.simiyu@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690. Tufuate kwa Telegram: Tuko news.

Post a Comment

0 Comments