SINTO SAHAU SIKU NILIYELALA NA MKE WA MPANGAJI MWENZANGU


Nikiri kwamba hakuna kitu nilichowahi kufanya kikanikosesha amani kama kulala na mke wa mtu.

Ilikua hivi,huyo mwanamke alikua mpangaji mwenzangu,mme wake alikua yupo huko mikoani,alikua mara kwa mara anatengeneza mazingira ya kuliwa,mara anitanie,hivi na vile nk.

Kufupisha story,alikuja siku moja rum kwangu,akanitega nikategeka,tukalala,baada ya kumlala nafsi yangu ilikosa amani,nikajuta,nikaona dunia nzima imeniona,ilikua usiku nikaona kama ni mchana,nikatamani nikimbie usiku huo,nikafunga mizigo yangu usiku huo huo nihame,nikaona kama dunia nzima imenielemea mimi.

Nikajuta usiku kucha,sikulala,asubuhi sa 11 nikaondoka kutoka nyumbani na kibegi kidogo cha mgongoni nikimbie aibu,nikawa na wasiwasi na mashaka yasioisha,naona kama kila mtu anajua,nikaenda stendi ila sijui naenda wapi,baadae nikaenda kwa rafiki yangu,nikalala mchana kutwa.

Niliposhtuka kama sa 10 jioni nawasha sim nakutana na meseji za yule mwanamke akinisifia sijui najua kufanyaje,kidogo akapiga sim,nikaikata,hofu yangu ikaongezeka mara dufu. Sikurudi nyumbani kama wiki nzima niko kwa rafki yangu.

Nikabadili namba ya sim ili yule mwanamke asinipate,sijui aliitoa wapi tena namba yangu mpya,kunichanganya zaidi akaniambia hajaona siku zake,nikachanganyikiwa,nikatam an dunia ipasuke niingie,nikawa na mawazo ya kujinyonga(kumbukumbu haikuja kama nilitumia mpira,kumbe nilitumia)

sitasahau hilo tukio,kwa kweli kulala na mke wa mtu ni vibaya sana,hata Bible imekataza hiyo dhambi. Kati ya dhambi zote nilizowahi kufanya hii ndio ilinikosesha amani,wala sitakuja tena kuirudia

Post a Comment

0 Comments