Penzi la Esma, Petit la mwendokasi


WANANZENGO wanasema eti wanandoa walioachana na kisha kurudiana, Esma na Petit safari hii penzi lao limekuwa na kasi kama ya mwendo kasi. “Yaani hii ni hatari, wenzetu utadhani ndiyo wamejuana leo kwa jinsi walivyofufua penzi lao, watu hatunywi maji mh! Hili penzi safari hii ni la mwendokasi,” alichangia mdau mmoja mtandaoni anayejiita Kidani.

Mbali na huyo, kurasa mbalimbali za wambea mitandaoni walichukua pichampya za wawili hao na kuzisambaza huku baadhi yao wakiwapongeza kwa kurushisha mahusiano yao na sasa walee vyema mtoto wao waliyempata kabla ya ndoa kuvunjika. Wawili hao waliachana, Petit akaoa mke mwingine lakini kwa sasa amemuacha na amerejesha majeshi kwa Esma

Post a Comment

0 Comments