BINTI AAMUA KUJIOA BAADA YA KUKOSA MUME WA KUMUOA

Binti mmoja amewashangaza wengi baada ya kuamua kujioa kupitia harusi iliyofana sana.

Amini usiamini, Georgina Wambui, alifanya harusi ya kukata na shoka ambapo alijioa mwenyewe na kuiacha familia yake vinywa wazi.

Georgina Wambui akiongea na Lyn Ngugi (kulia) wa TUKO.co.ke wakati akimhoji. Picha: Edwin Ochieng

Dada huyo mwenye umri wa miaka 33 alielezea TUKO.co.ke kwamba alikuwa na mpenzi siku za awali lakini penzi lao likasambaratika na akaanza kuishi bila ya mume.

Mambo yalizidi kuharibika 2014 baada ya kuhusika katika jali iliyomwacha na majeraha mabaya ambayo hadi leo yamemfanya kuwa mlemavu.

"Baada ya ajali, niliwapoteza marafiki wengi ambao walikuwa karibu na mimi. Jambo hilo lilinibadilisha sana na kunipa nguvu. Niligundua si marafiki wote wa kudumu," alisema katika mahojiano na mwanahabri wetu.

Georgina Wambui wakati wa harusi yake. Alifanya harusi na kujioa katika hafla iliyowashangaza wengi. Picha: Edwin Ochieng

Mnamo Juni 1, 2018 familia yake ilishangaa sana wakati aliposherekea siku ya kuzaliwa kwake kwa kujinunulia pete na kuwaeleza marafiki kuhusu mapango wa kutaka kujioa mwaka uliofuata.

Ahadi hiyo ilitimia Juni 1, mwaka huu alipofanya harusi.

"Niliamua kufanya hivyo ili kutosheleza nafsi yangu na ila si eti siamini kuna penzi. Nashabikia ndoa pia lakini nimefanya nipendalo na wala si kulingana na vile jamii inataka," alisema.

Georgina Wambui wakati wa harusi yake ambapo alijioa mwenyewe. Picha: Edwin Onyango

Wambui aliongeza kuwa alikuwa na matumaini mengi ya kuolewa lakini hakuna mtu aliyejitokeza kumrushia ndoano.

"Unaweza kuwa umeamua kusubiri, lakini utasubiri mtu maisha yako yote? Nilitaka sana nimpate jamaa anioe lakini sasa hakuna aliyejitokeza," aliongeza kusema.

Licha ya kujioa, dada huyo alisema ana matumaini ya kupata mtoto.

Post a Comment

0 Comments