Sifa zitakazokuonesha mwanamke ambaye ni sahihi zaidi kwako



Katika  maisha haya  ya kila siku hususani katika kipengele cha  kimahusiano, wanaume  wengi huwa wanakutatana na wanawake wa aina tofauti tofauti, ila wengi wao bado hawajatambua ni yupi hasa ni mwanake sahihi katika maisha yao. Makala ya leo inakuangazia sifa ambazo zitakuonesha mwanamke ambaye  ni sahihi zaidi kwako kama ifutavyo:

1. Mwanamke ambaye ni mkweli.

Mwanaume, endapo utakutana na mwanamke ambaye ni mkweli basi anza kutangaza ndoa kabisa, hii ni kwa sababu katika maisha haya ni asilimia chache sana kumpata mwanamke ambaye ni mkweli, wengi wao maisha yao huwa yanaongozwa na dhana ya uongo kwa asilimia kubwa.

Hivyo mwanamke mwenye mapenzi ya dhati na wewe mara nyingi huwa haoni aibu kukwambia ukweli kwa yale yanayomsibu na yale yaendeleayo katika mahusiano yenu, pia daima ikumbukwe kuwa ukweli na uwazi hufanya mapenzi yadumu daima.

2. Mwanamke mwenye mawazo chanya.

Katika maisha haya endapo utapata mwanamke mwenye mawazo chanya basi huyo ndiye atayekufaa maishani. Mwanamke mwenye kujua nini maana ya maisha huyu ndiye mke bora kwako, mwanamke mwenye kukushauri mbinu mbalimbali za kuweza kufanikiwa kwenu basi huyu ndiye mwenye dhamana kubwa zaidi kwako.

Kila wakati ukiwa na mwanamke wa aina hii basi huyu ni mtu sahihi zaidi kwako, na aina hii ya wanawake ndiyo wale waliandikwa kwenye vitabu vya dini kuwa kila palipo na mafanikio ya mwanaume basi nyuma yake pana mwanamke.

3. Mwanamke mwenye mchango katika kufikia malengo yako.

Ukipata mwanamke mwenye kuchangia mawazo yake katika kukamilisha mipango yako basi huyu ndiye wife material. Mwanamke mwenye kukupa ushari labda tungefanya hivi ingekuwa vile basi huyu usije ukamuacha aende zake kwa sababu hawa ni wanawake wachache sana waliopo kwenye ulimwengu huu na wanagombaniwa sana.

Hizo ni baadhi za sifa chache kati nyingi ambazo zitakuonesha sifa za mwanamke ambaye anakufaa kuwa naye, Endelea kutembelea Muungwana blog.

Na. Benson Chonya.

    

Post a Comment

0 Comments